Waziri Mkuu aliyeteuliwa DK Ruhakana Rugunda (kushoto) ambaye amebadili nafasi Amama mbabazi (Kulia).Rais wa Uganda Yoweri Museveni amemfuta kazi waziri mkuu, Amama mbabazi na kumteua Dk Ruhakana Rugunda kushika wadhifa huo .
Taarifa elekezi ya Rais Museven kwenda kwa spika wa Bunge Rebecca Kadaga, kwa njia ya barua imeeleza nia ya mabadiliko hayo na kuambatanisha
pia uteuzi wa Dk Rugunda
Rais Museven amemshukuru Mbabazi kwa mchango wake kwa nchi ya Uganda tangu mwaka 2011 akieleza kuwa ujuzi na uongozi bora aliokuwa nao
utaendelea kuigwa na kuwa chachu ya uongozi bora kwa manufaa ya watu wa Uganda. (FS)
Bwana Mbabazi alikuwa anatarajiwa na wengi kuwa mpinzani wa Museveni katika uchaguzi ujao. Waziri mkuu anayeondoka Amama Mbabazi
alionekana kuwa angemrithi rais Museveni lakini miaka mitatu ambayo amehudumu katika wadhifa
huo uhusiana kati yake na Museveni haujakuwa mzuri.
Mapema mwaka huu chama kinachotawala kiliidhinisha azimio kikisema kuwa rais Museveni
ambaye amekuwa kiongozi kwa muda wa miaka 28 atakuwa mgombea wake wa pekee kwenye uchaguzi
wa mwaka 2016.
Hata hivyo mkewe Mbabazi ambaye pia ni afisa wa cheo cha juu chamani amesema kuwa mmewe ameonewa.
Waziri mkuu mpya ambaye ni mtaalamu wa masuala ya afya awali alikuwa amehudumu kama waziri wa
afya. Daily Monitor
Chapisha Maoni