0
BAADA ya ukimya wa muda mrefu huku ikidaiwa kuwa staa wa Mduara Bongo, Snura Mushi amepachikwa ujauzito, meneja wa msanii huyo, Mohamed Kavu ‘HK’ amezidi kuyeyusha ukweli na
kudai msanii wake hana mimba.]


Akizungumza na paparazi wetu mara baada ya uchunguzi makini kufanyika na kubaini staa huyo amehamia kwa mpenzi wake mkoani Mbeya,
meneja huyo alikataa katakata kuwepo kwa suala la ujauzito.

“Hana mimba. Yupo Afrika Kusini, anashuti video yake lakini tunatarajia baada ya wiki mbili atakuwa
amerudi.” Staa wa Mduara Bongo, Snura Mushi.
Badala ya wiki mbili, paparazi wetu alimpa meneja huyo mwezi mzima lakini hakutokea, alipoulizwa kwa mara nyingine, alisema Snura alitarajiwa
kuingia Bongo juzi, Oktoba 16. Tunaendelea kufuatilia.

Kwa muda mrefu Snura amekuwa kimya pasipo kuposti kitu kwenye mitandao ya kijamii wala kufanya shoo ya aina yoyote.

Chapisha Maoni

 
Top