Wananchi wakiwa wamemzungukaKakakuona aliyeonekana asubuhi majira ya saa moja maeneo ya Kigamboni Kisiwani.
Mtaa wa Chaboko ambapo kwa mujibu wa ripota na mpiga picha wetu Salma Bob Kassim, mnyama huyo aliwekewa Unga, ndizi, maji pamoja na pesa.
Lakini akaishia kunywa maji tu kabla ya
kukimbilia vichakani. Wananchi kwa
mamia waliofurika kumuona Kakakuona
huyo walisikika wakisema kuwa huenda
huo ni utabiri kwamba huenda mvua
zikawa nyingi msimu huu.
Polisi walifika eneo la tukio na baada ya
kuona hakuna uvunjifu wa amani wakatoa taarifa kwa maafisa wa Maliasili ambao walifika na kumtia mnyama huyo kwenye kiroba na kuondoka naye
Kakakuona akijikunja baada ya umati wawatu kuzidi kuwa mkubwa
Baadaye, huku mvua kubwa ikiendeleakunyesha, Kakakuona huyo alielekea
vichakani huku umati ukiendelea
kumshangaa. Baadaye watumishi wa
Maliasiali walifika na kumtia kwenye
kiroba na kuondoka naye.
Chapisha Maoni