Binti Mrembo ndani ya Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefafanua ukaribu wake na Martin Kadinda kwa kudai ni rafiki yake wa karibu nahakuna cha ziada.
Akizungumza na mwandishi wetu, Lulu alisema yeye na Kadinda ni marafiki wa kweli na amekuwa akiyafurahia maisha yao kwa kushauriana masuala mbalimbali ya kimaisha tofauti na
wengine wanavyojiongeza.
“Kadinda ni mtu wangu wa nguvu hakuna kingine zaidi ya urafiki wa kawaida, manenomaneno ni
kawaida kwa wanadamu,” alisema Lulu.
Chapisha Maoni