0
MSHAMBULIAJI Wilfried Bony amekamilisha uhamisho wa dau nono kutoka Swansea kwenda kwa mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester City.

Mpachika mabao huyo wa Ivory Coast, ambaye yupo na timu yake ya taifa kwa sasa kwa maandalizi ya Fainali za Mataifa ya Afrika, anajiunga na kikosi cha Manuel Pellegrini kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 25 huku
Pauni nyingine Milioni 3 zikiongezeka katika Mkataba huo wa zaidi ya miaka minne.

Bony, mwenye umri wa miaka 26, amekubali mkataba wa miaka minne na nusu na atakuwaanavalia jezi namba 14, ambayo awali ilikuwa
inavaliwa na Javi Garcia.

Wilfried Bony amejiunga na Manchester City kwa mkataba wa miaka minne na kukabidhiwa jezi namba 14

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 hapa anasaini Mkataba wa kujiunga na Manchester City

Wilfried Bony akiwa na Rais wa Ivory Coast, Sidy Diallo baada ya kukamilisha uhamisho wake Manchester City

"Ni hisia babu kubwa kwangu, ni heshima kubwa kuwa hapa na ni changamoto kubwa,"amesema Bony akiwa mwenye furaha.

"Kama mchezaji wakati wote ni vizuri kuwa sehemu ya klabu kubwa duniani na ni fursa nzuri kwangu kuwa katika mazingira hayo – ninajivunia sana hilo,".
"Najisikia faraja sana kusubiri zama hizi mpya zifike, ni babu kubwa. Nafikiri ni uamuzi babu kubwa kwangu - Manchester City ipo katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Unakumbuka mwishoni mwa msimu uliopita nilisema kwamba kama ninataka kuhama, itakuwa kwenye timu inayoshiriki mashindano hayo, kwa sababu ni michuano mikubwa ambayo ninataka haswa kucheza na kushinda pia,:.

Chapisha Maoni

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top