Azam FC imesema kwamba ipo kwenye mazungumzo na wachezaji wake wawili wanaohusishwa na mpango wa kutaka kuhamia Simba, kipa Aishi Manula na beki, Shomary Kapombe.
Wawili hao wote wanamaliza mikataba yao mwezi huu na imekuwa ikiripotiwa kwamba wako kwenye mipango ya kujiunga na Simba SC. Msemaji wa Azam, Jaffar Iddi amesema mazungumzo yanaendelea na watasaini mkataba mpya.
Chapisha Maoni