Waziri wa Fedha na Mipango nchini, Dkt. Philip
Mpango, amefafanua adhabu ya kosa la kutotoa
ama kudai risiti katika manunuzi na kusema kuwa
serikali imefuta kipengele cha kufungwa na pia
faini itatozwa kulingana na ghamara ya bidhaa
itakayonunuliwa.
Akizungumza leo Mjini Dodoma na kupitia Shirika
la Habari la Taifa, Dkt. Mpango amesema kuwa
wameamua kufanyia marekebisho sheria hiyo
kutokana na maoni ya wadau mbalimbali lakini
bado adhabu itatolewa kwa mtu yeyote asietoa
ama kudai risiti wakati wa mauzo.
Dkt. Mpango amesema kuwa moja kati ya faida
kwa wafanyabishara katika kutoa risiti ni pamoja
na kuweka rekodi nzuri katika biashara lakini pia
na mnunuzi kujua ni kiasi gani umekatwa kwa
ajili ya kodi.
Amesema kuwa sheria waliyoiweka sasa adhabu
itatolewa kutokana na ukubwa wa mauzo ya
mfanyabiashara ili kuwalinda wafanyabiashara
wadogo ambao watakuwa wanatenda makosa
hayo ili kuwakumbusha umuhimu wa kutoa risiti
katika mauzo yao.
Ameeleza kuwa lengo kuu la kufanya hivyo ni
kujenga taifa lenye utamaduni wa kulipa kodi
lakini pia fedha hizo zitasaidia miradi mbalimbali
ya maendeleo ikiwemo katika sekta ya Afya, Elimu
na maeneo mengine.
Dkt. Mpango amesema kuwa wapo
wafanyabiashara wengine wanauza mamilioni ya
shilingi lakini hawatoi risiti za mauzo yao jambo
ambalo linaikosesha serikali mapato halali na pia
mnunuaji anakua hajui ni kiasi gani cha kodi
amekatwa kutoka na manunuzi ya bidhaa hizo.
Related Posts
Tumuombee duwa njema mzee wetu Kig Majuto
Msanii maarufu wa maigizo Amr Athuman ‘King Majuto’ amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimb[...]
Aug 03, 2018Korea kaskazini kuchukua hatua
Korea kaskazini imesema itachukua hatua dhidi ya kutumwa kwa mfumo wa hali ya juu kuzuia [...]
Jul 11, 2016Shilingi bilioni 1.3 zakusanywa daraja la Nyerere
Jumla ya shilingi bilioni 1.3 zimekusanywa kutoka Daraja la Nyerere lililopo Kigamboni jijini Dar [...]
Jul 11, 2016RAIS MAGUFULI AMPOKEA WAZIRI MKUU WA INDIA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM
1.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea Waziri Mkuu wa India Na[...]
Jul 10, 2016Jeshi la Polisi Latoa ONYO Kali Kwa Vyama vya Siasa
ONYO limetolewa kwa vyama vya siasavinavyojaribu kusuguana na Jeshi la Polisikukumbuka kuwa hilo n[...]
Jul 10, 2016Haki sawa Wanawake walia Magufuli ‘kuwabania’ katika uteuzi
Mashirika yanayotetea haki za wanawake nausawa wa kijinsi nchini yamesema uteuzi wanafasi muhimu z[...]
Jul 10, 2016
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Chapisha Maoni
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.